Search This Blog

Wednesday, February 20, 2013

Chadema, NCCR Mageuzi wang’aka juu ya matokeo ya Form IV



Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Jemes Mbatia akiwaonyesha waandishi wa habari, kitabu cha mitalaa ya Elimu ya Sekondari, alipokuwa akizungumza kuhusu kushuka kwa kiwango cha elimu nchi. 

Umeisikia hiyo “Chadema, NCCR Mageuzi wang’aka

Umefika wakati wa kuweka tofauti zetu za kisiasa pembeni, tufanye kazi kwa pamoja ili kulinusuru taifa letu na elimu hii ya maafa, nilishangazwa sana na kitendo cha wabunge wa CCM kuipinga hoja yangu, haya ndio matokeo sasa haya yote yalitolewa na Mh. James Mbatia

Je.! huu ni uungwana...??

Wanaume muwenahuruma kwa kwamanawake wenu. 
Utakuta dume zima full kumnyanyasa binti wa watu, utampendaje mwanamke bila kumjali bhana,? yaani we unapenda penda tu,  ukimwona kapendeza hujui amejigalimiaje,  we unatungua na kumweka ndani bila kujali thamani yake, unafikiria imekuwa nguo hiyo. haya sasa unajikuta unamshindisha njaamrembo wa watu na kuwaachia majukumu watu wengine buree!! kisha jioni wataka Game du. Hivi wengine wakikusaidia kulea utalaumu…?? Ebo….. Mzee mzima Nay Wa Mitego hajakosea kabisa wanaume wote mlaaniwe mnaowanyanyasa wanawake na malaaniwe
Hata kwenye vitabu vya dini imeandikwa mwanamke ni dhaifu sana unapompiga na kudhalilisha unakosea bana iweje umdhalilishe iweje leo mnyanyase ........ kamaumemchoka mwana wa mwenzio basi umrudishe kwao ni wanaumefeki hao wanaowanyanya wanawake wanake zao

Tuesday, February 19, 2013

MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (FORM IV) 2012


The National Examinations Council Of Tanzania (NECTA) 
Balaza la Mitihni Tanzania (BAMITA)
 
Matokeo ya mtihani wa kidato cha Nne ( Form IV ) 2012
 

Hatimaye baadaya wanafunzi kuwa na hamu ya kupata matokeo yao ya kidato cha nne balaza la mitihani la toa matokeo hayo katika mtandao wao, kwa hupata matokeo hayo tembelea mtandao wa balaza la mitihani kwa hubofya hapa

Saturday, February 16, 2013

Ajira! ajira! ajira!

Kwa wale ambao walioomba ajira katika wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi  nchini Tanzania  hatimaye wizara hiyo imeamua kutoa ajira kama ilivyo tarajiwa. 

AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHAHADA WA SHULE ZA SEKONDARI MWAKA 2012/13. bofya hapa kuyapata majina hayo.

AJIRA MPYA YA WALIMU WA VYUO VYA UALIMU NA SHULE ZA MAZOEZI MWAKA 2012/13  bofya hapa kupata list ya majina hayo.

Wizara hiyo imetoa taarifa kuwa.

Walimu wote waliopewa ajira ya Ualimu Serikalini ambao majina yao yametangazwa katika tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI, wanatakiwa kuripoti tarehe 01 Machi 2013 kwenye Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri walikopangiwa kwa ajili ya kupangiwa Vituo vya kazi. HAKUNA MABADILIKO YA VITUO VYA KAZI YATAKAYOFANYWA. Mwalimu anatakiwa kwenda na vyeti vyake halisi vya taaluma na cheti cha kuzaliwa pamoja na nakala zake. Mwalimu ambaye hataripoti ifikapo tarehe 9 Machi 2013 atapoteza nafasi hiyo. NB: WALIMU WALIOKWISHA AJIRIWA WARUDI KWA WAAJIRI WAO
 

Thursday, February 14, 2013

Vikao vya bunge kutorushwa Live.


No' Wabunge kutokelezea live! live! kwenye kideo hukuwakioneshana mnjonjo yao na Watanzania wakiwakodolea mcho waziwazi. Umelifahamu hili



Kwa lengo la kukomesha vurugu za wabunge wanaotafuta umaarufu .Bunge lianza mchakato kusitisha matangazo ya vikao vyake kurushwa moja kwa moja yaani live  kama ilivyo kawaida ya bunge hili. Imedaiwa kuwa itarushwa  katika mfumo wa yaliyojiri katika vikao hivyo baada ya kuhaririwa, na hii yote imetokana kuwa bunge haliendeshwi kwa kanuni, wabunge wanamasilahi yao  binafsi na kuwa bunge  siyo kilabu au mahali pa kuoneshana ubabe hivyo lengo hili ni kwaajiri ya kuweka utaratibu mzuri wa matukio bungeni  hapo  haya yote yamejili hapo bungeni.
Lakini swala la kujiuliza hivi kweli kutorushwa live kwa matukio hapo bungeni kunafuata sera nzima za Demokrasia ? 

Matokeo ya Sensa ya watu na Makazi 2012



MATOKEO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI YA 2012( 31.12.2012) ILIVYOTOLEWA NA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE.


                         Kwa mjibu wa sensa ya watu na makazi ya 2012 sasa Tanzania ina watu Wapatao 44,929,002.Tanzania Bara ni watu 43,625,434 na Zanzibar ni watu 1,303,568.
Sensa hii ilifanyika Agosti 2012.Kabla ya uhuru sensa y kwanza Tanganyika ilifanyika 1910 na 1957 na Zanzibar 1958.Kwa Tanzania Bara baada ya uhuru sensa ya kwanza ilifanyika mwaka 1967 Tanzania Bara watu walikuwa 11,958,654 na Zanzibar walikuwa watu 354,400 jumla kuu ilikuwa 12,313,054, ya pili mwaka1978, ya tatu mwaka 1988, ya nne mwaka 2002 na tano ni mwaka huu 2012 agosit.Sensa ya2002 watu walikuwa 34,400,000.Sensa hii ilifanyika kwa watu wote waliolala usiku wa kuamkia agosit26 2012.

Monday, February 4, 2013

Msanii mwenye kipaji cha ajabu..!


Wamfahamu msanii huyu ajulikanaye kama Paul Timoth. anayefahamika kama Mwasile




Mwasile


da duniani kunawatu wenye vipaji cheki na Msanii huyu