Search This Blog

Saturday, February 16, 2013

Ajira! ajira! ajira!

Kwa wale ambao walioomba ajira katika wizara ya Elimu na Mafunzo ya ufundi  nchini Tanzania  hatimaye wizara hiyo imeamua kutoa ajira kama ilivyo tarajiwa. 

AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHAHADA WA SHULE ZA SEKONDARI MWAKA 2012/13. bofya hapa kuyapata majina hayo.

AJIRA MPYA YA WALIMU WA VYUO VYA UALIMU NA SHULE ZA MAZOEZI MWAKA 2012/13  bofya hapa kupata list ya majina hayo.

Wizara hiyo imetoa taarifa kuwa.

Walimu wote waliopewa ajira ya Ualimu Serikalini ambao majina yao yametangazwa katika tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu- TAMISEMI, wanatakiwa kuripoti tarehe 01 Machi 2013 kwenye Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri walikopangiwa kwa ajili ya kupangiwa Vituo vya kazi. HAKUNA MABADILIKO YA VITUO VYA KAZI YATAKAYOFANYWA. Mwalimu anatakiwa kwenda na vyeti vyake halisi vya taaluma na cheti cha kuzaliwa pamoja na nakala zake. Mwalimu ambaye hataripoti ifikapo tarehe 9 Machi 2013 atapoteza nafasi hiyo. NB: WALIMU WALIOKWISHA AJIRIWA WARUDI KWA WAAJIRI WAO
 

No comments:

Post a Comment